Sunday, July 29, 2012

Tigo Wanasema :- Jihadhari Na Vocha Zilizotumika...!



JITAHADHARISHE NA VOCHA ZILIZOTUMIKA

Kuna njia mpya unatumika na vibaka na wezi wa magari kutoweka kwenye mkono wa sheria kutokana na uhalifu wao. Wanakusanya vocha zilizotuma pindi wanapotelekeza gari au kutupa miili ya watu waliokufa na kuacha vocha hizo zilizotumika kwenye tukio.
Polisi wakifika eneo la tukio wanatumia namba za hizo vocha kusaka namba ya simu yamtumiaji wa hiyo vocha. Tayari watu wawili wameshikiliwa keko wameathirika na huu udanganyifu. Tafadhali hakikisha umeharibu vocha yako baada ya kutumia ili nawe usipatwe na janga hili.
Taarifu habari hii na marafiki zako
Pichani Mh. Kabati akimkabidhi msaada wa jezi Francis Godwin, mratibu wa klabu ya mpira ya TASWA, Iringa. Franchis pia ni bloga mahiri na anamiliki blogu yake ya Francisgodwin.blogspot.com



Na Mwandishi wetu Iringa



Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati (CCM) na mbunge wa jimbo la Ismani Wiliam Lukuvi wameanza kuisaidia jezi seti moja moja timu ya waandishi wa habari za michezo Tanzania (TASWA) mkoa wa Iringa kama njia ya kuiunga mkono timu hiyo katika kuhamasisha michezo mkoani Iringa.

Akikabidhi msaada huo leo kwa mwenyekiti wa TASWA mkoa wa Iringa Francis Godwin ,mbunge Kabati alisema kuwa amelazimika kutoa msaada huo kama sehemu ya kuunga mkono unzishwaji wa timu hiyo .

Kwani alisema suala la michezo lime katika ilani ya uchaguzi wa CCM hivyo akiwa kama mbunge ameguswa na mkakati wa wanahabari mkoa wa Iringa katika kuhamasisha michezo na kuwa miongoni mwa wadau wa kweli wa michezo ambao wamekuwa wakiandika habari za michezo ila pia na wao wenyewe kuonyesha mfano katika michezo kwa kuwa na timu yao.

Mbunge Kabati alitoa wito kwa wabunge wengine na wadau wa michezo katika mkoa wa Iringa kujitokeza kuisaidia timu hiyo vifaa vya michezo pamoja na misaada mbali mbali pale inapohitajika ili kuiwezesha kuwa timu bora katika mkoa wa Iringa.



Kabati alisema kuwa bado ataendelea kuisaidia timu hiyo ya TASWA pamoja na kuisaidia vifaa zaidi vya michezo kwani imeonyesha mfano mwema kwa makundi mengine ya kijamii katika mkoa wa Iringa.



Mbali ya kuahidi kuendelea kuisaidia timu hiyo bado alisema anaiandalia safari ya kwenda bungeni Dodoma ili kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na kuitambulisha rasmi kwa wabunge wa mkoa wa Iringa na wabunge wengine ila nao kuanza kuzisaidia timu kama hizo katika mikoa yao.



Hata hivyo alimpongeza mwenyekiti wa TASWA Iringa Francis Godwin kwa kuanzisha mkakati huo mzuri wa kuwa na timu ya pamoja na wanahabari wote itakayojenga umoja na mshikamano miongoni mwa wanahabari mkoa wa Iringa.



Mbunge Kabati alisema kuwa pamoja na kuisaidia jezi timu hiyo ya TASWA pia amekuwa akisaidia vifaa vya michezo timu mbali mbali za vijana katika jimbo la Iringa mjini na majimbo mengine yanayounda mkoa wa Iringa na kuahidi kuendelea kufanya hivyo kwa vijana wote ikiwa ni pamoja na kuwaahidi vijana hao kuwaunganisha kupitia tamasha kubwa la michezo ambalo litafanyika hivi karibuni mjini Iringa kwa vijana wa mkoa mzima wa Iringa.



Kwa upande wake mwenyekiti wa TASWA Iringa Francis Godwin akishukuru kwa msaada huo alisema kuwa mbunge huyo ameonyesha mfano kwa wabunge wengine na wadau wa michezo katika kuisaidia timu hiyo na kumwomba kuwa mlezi wa timu hiyo .



Godwin alisema kuwa mbali ya mbunge Kabati kusaidia seti hiyo ya jezi pia mbunge wa jimbo la Ismani Wiliam Lukuvi ambaye ni waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera na uratibu wa bunge pia ameisaidia timu hiyo jezi seti moja na kuwa jezi hizo zote zitakumbukwa na TASWA kwa kuandikwa majina yao nyuma ya jezi hizo kama njia ya kuwaenzi kwa mchango wao huo.



Hata hivyo alisema kwa sasa timu hiyo inakabiliwa na ukata wa fedha kwa ajili ya kusafirisha timu hiyo kwenda kucheza mechi za kirafiki na timu za nje ya mji wa Iringa ,pamoja na viatu vya wachezaji na hivyo kuwaomba wadau wengine kujitokeza kuendelea kuisaidia zaidi.



Wakati huo huo Godwin alisema kuwa timu hiyo ya TASWA 2012 itazinduliwa rasmi siku ya jumapili katika uwanja wa Samora mjini Iringa kwa mchezo wa kirafiki kati ya waheshimiwa madiwani na wanahabari hao hivyo kuwataka wanahabari mkoa wa Iringa kuendelea kujitokeza kwa wingi katika mazoezi yanayoendelea katika viwanja vya Kleruu kila siku majira ya saa 11 .30 jioni .

MWEZI MTUKUFU: Machangu wala Kichapo na Mboko za Nguvu huko Kinondoni Ni Kutoka Kwa Kikundi Cha Jumuia Ya Uamsho Tanzania Bara!

Stori: Issa Mnally na Richard Bukos
Machangu wamekiona cha mtemakuni! Wakati Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ukiwa katika chungu cha nane, akina dada wanaofanya biashara haramu ya kuuza miili maarufu kama Machangudoa au Chipsi Funga au Wauza Sukari Tamu, wamekula viboko laivu baada ya kutuhumiwa kuwatega Waislamu.
Tukio hilo lilijiri katikati ya wiki hii ambapo vijana wa Kiislamu waliodai ni wa kikundi cha Jumuiya ya Uamsho Tanzania Bara walizunguka mitaa mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam na kuwashushia fimbo machangu ambao kwa sasa wametapakaa kila kona jijin
WATUMIA BAJAJ
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, waumini hao, wakiwa wamevaa kanzu huku wakitembea na bakora mkononi walichukua jukumu la kukodi Bajaj na kuzunguka maeneo mbalimbali jijini inapofanyika biashara hiyo haramu ya ukahaba.
BARABARA YA SHEKILANGO
Vijana hao waliolenga kukomesha biashara hiyo hasa kipindi hiki cha mfungo walianzia kwenye Barabara ya Shekilango inayokatiza kwenye viunga vya Sinza, Dar ambapo kila kituo cha daladala kuanzia Afrika Sana hadi kwenye mataa ya Shekilango waliwakuta machangu na kuwatandika viboko kabla ya kutua mitaa ya Mwenge.
KINONDONI
Baada ya kufagiafagia Sinza kwa kuwaadabisha wanawake hao ndipo zoezi likahamia mitaa ya Kinondoni ambapo nao walipokea bakora za kutosha huku wengine wakitoka nduki.
KISA KUHARIBIWA SWAUMU
Kwa mujibu wa vijana hao, walifikia hatua ya kufanya zoezi hilo baada ya muumini mmoja wa kiume kukatiza maeneo ya Corner Bar, Afrika Sana na kuvutwa kisha kuchezewa nyeti na makahaba na kusabisha kuharibika kwa swaumu yake.
Ilielezwa kuwa baada ya kukutwa na kimbembe hicho, ilibidi muumini huyo kukatiza safari yake ya kwenda kuswali msikikini mishale ya saa 2:00 usiku.
Ilisemekana kuwa aliporudi nyumbani alitawadha na kufunga safari nyingine ya msikitini na alipofika kwenye nyumba hiyo ya ibada ndipo akawasimulia waumini wenzake ambao nao walikasirishwa na kitendo hicho hivyo wakapanga kuvamia maeneo yote ya biashara hiyo ili kuwashikisha adabu.
Waandishi wetu, wakiwa kwenye mishemishe zao za kutafuta habari mishale ya saa 5 usiku waliwashuhudia waumini hao wapatao saba wakishuka kwenye Bajaj nyeusi maeneo ya Sinza wakiwa na bakora mikononi kisha kuwavaa machangu hao na kuwatandika.
Wakati wakitekeleza zoezi hilo, jamaa hao walisikia wakiwaambia: “Sisi tupo kwenye swaumu nyiye mnatutega, ala!”
HAWAHESHIMU MWEZI MTUKUFU?
Waumini hao waliongeza kuwa makahaba hao wamekuwa hawaheshimu mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan ndiyo maana wanaendeleza biashara yao hiyo ya aibu.
www.globalpublishers.info

Mashambulio ya Aleppo ni ya kusita-sita

Wanajeshi wa serikali ya Syria wameendelea na mashambulio yao dhidi ya maeneo yanayodhibitiwa na wapiganaji katika mji wa Aleppo.
Inaarifiwa kuwa watu zaidi ya 30 wameuwawa.
Lakini inaonesha jeshi la ardhini la Syria halijaweza kusonga mbele katika baadhi ya mitaa, na mwandishi wa BBC anasema,
inaonesha vita vya Aleppo kwa sasa ni vya mashambulio ya mizinga na mabomu kila baada ya muda.
Katika eneo la Deir ez-Zor, wanaharakati walisema watu 17 waliuwawa wakati vifaru vilivopiga basi ambalo lilikuwa na watu waliokuwa wakikimbia mapigano.

Thursday, July 26, 2012

Ukimwi Siyo Tishio Tena Duniani

WANASAYANSI mbalimbali wanaoendesha tafiti mbalimbali za kutafuta tiba na chanjo ya Ukimwi, wameitangazia dunia kuwa hatua waliyofikia sasa wanauona ugonjwa huo ‘siyo hatari tena’ kwa sababu wanazo silaha zote za kuweza kukabiliana nao.

Ila wakasema, kinachowakwamisha ni ukosefu wa fedha ambazo zinahitajika katika kuendeleza tafiti na kuweka sera mpya za kukabili Virusi Vya Ukimwi (VVU) duniani.

Hayo yalibainika kwenye siku ya pili ya Mkutano wa 19 wa Kimataifa wa Ukimwi unaofanyika mjini Washington DC, Marekani na unahudhuriwa na watu zaidi 22,000 miongoni mwao wakiwamo wataalamu wa afya, watunga sera na wadau wa mapambano dhidi ya ugonjwa huo toka karibu kila kona ya dunia.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Kitengo cha Habari cha Mkutano huo na gazeti hili kufanikiwa kupata nakala yake, ilieleza kwamba jopo la wanasayansi nguli duniani walikiri kuwa wamefanyia VVU utafiti wa kutosha ndiyo maana wanatamba kuwa wamefanikiwa katika kuvidhibiti.

“Kwa sasa tunazo silaha zote za kisayansi kumalizia mbali gonjwa hili la Ukimwi. Kilichobaki ni kutumia kikamilifu utaalamu huu katika fursa hii tuliyo nayo,” alisema Rais wa Taasisi ya Kijamii ya Kimataifa ya Mapambano dhidi ya VVU (IAS), Dk Elly Katabira.

Nafasi Ya Wataalamu Katika Biashara

Na: Meshack Maganga-Mjengwablog,Iringa.

Kwa muda mrefu sasa nimejijengea utamaduni imara wa kujisomea vitabu. Sisomi kila aina ya vitabu, isipokuwa ninapenda sana vitabu vya biashara na uchumi (finances, economic, entrepreneurship and business) pili ni vile vya mahamasisho na shuhuda (motivational and inspirational) na vingine ni vile vinavyohusu ustawi wa kiroho na kimaisha (spiritual and personal improvements). Mara chache sana huwa navisoma vitabu vinavyohusu siasa.

Nimejiwekea ratiba ya kusoma angalau vitabu viwili kila mwezi ambayo ni idadi ya vitabu ishirini na nne kwa mwaka. Pia ni msikilizaji mzuri wa rekodi za sauti zenye maudhui kama ya vitabu nilivyovitaja. Pamoja na kusoma kote huku vitabu huwa nina mchujo mkali sana wa vitabu vya kusoma kutegemea na sifa za mwandishi husika.

Daima huwa nasoma kazi za waandishi ambao wamepitia kwa vitendo waliyoyaandika na sio wale wanaoandika nadharia. Sisomi kazi za wenye vyeti vikubwa vya madarasani, ninasoma kazi za wenye uzoefu kwa yale waliyoyaandika kivitendo.

Ndio maana ninapenda sana vitabu kama ‘Retire Young Retire Rich’ (Robert Kiyosaki), ‘As A man Thinketh’ (Allen James), ‘Secrets of Millionaire Minds’ (Harv Eker), ‘Think and grow rich’ (Napoleon Hill) “Financial IQ” (Robert Kiyosaki), kwa kuvitaja kwa uchache. Nawapenda waandishi hawa kwa sababu wameandika kile walichokiishi. Huu ni mtazamo na msimamo wangu. (usijichoshe kuuhoji wala kuukosoa)

Ndio maana kila siku ninapojiuliza ni kwa nini tunazalisha wasomi wengi wenye vyeti katika maarifa ya biashara lakini hatuoni wakitumia elimu zao kuibua miradi, biashara na kutengeneza ajira; ninabaini kuwa moja kwa moja tatizo lipo kwenye mifumo yetu ya kielimu.

Ni vigumu sana profesa (ama mhadhiri) anaefundisha
kozi ya biashara chuo kikuu (ambaye hana hata banda la kuuzia chipsi) kuzalisha mjasiriamali/mfanyabiashara halisi. Anachoweza kufanya ni kuzalisha wenye vyeti wengi ambao wanabaki kuwa mzigo mitaani. Kama ambavyo huwezi kujifunza kuogelea kwa kusoma maandishi, pia haiwezekani kujifunza biashara kwa kusoma vitabuni pekee.

Kama inavyotakiwa kuingia majini na kuanza kugusa maji, ndivyo ilivyo hata kwa biashara, ni lazima uingie na kuionja. Mkufunzi wa uogeleaji atafanikiwa kuzalisha waogeleaji wengi na walio mahiri kwa kuonesha kwa vitendo namna ya kuogelea (ikiwemo upigaji mikono na urushaji miguu ukiwa majini).

Ndivyo ilivyo pia kwa wasomi wakufunzi wa mambo ya biashara na ujasiriamali. Hatuwezi kuzalisha wajasiriamali wa ‘ukweli’ ikiwa wanaowafundisha hawajawa mifano ya kuigwa (they are not role models). Hali hii tete inaibua tatizo jingine kubwa katika ujasiriamali wa kitanzania pale zinapohitajika huduma za kitaalamu ikiwemo ushauri wa kibiashara.

Kiukweli ushauri wa kitaalamu katika ujasiriamali na biashara unahitajika sana hasa katika nyakati hizi ambazo tunapambana na ushindani wa kimataifa. Unaposikia neno ushauri pamoja na mantiki yake ni kwamba huwa una machaguo matatu. Unaweza kuukataa wote, unaweza kuutumia wote ama ukachukua kidogo na kuikataa sehemu fulani. Yote katika yote ushauri wa kibiashara tunatazamia unapotumika ulete tija ya uboreshaji wa biashara ama eneo uliloshauriwa.

Biashara zinahitaji kuwa na michanganuo ya kitaalamu ambayo husaidia kukupa dira ya namna ya kutekeleza malengo yako. Michanganuo huweza kutoa mwangaza wa kujua ni wapi hapaendi sawa na mbinu gani zitumike kuokoa hali pale mambo yanapoenda hali jojo. Maeneo mengine yanayohitaji utaalamu ni katika uibuaji wa biashara mpya, utunzaji wa hesabu, uratibu wa masoko pamoja na upatikanaji wa mikopo na mienendo ya kodi.

Ukiniomba mimi nikushauri masuala ya biashara sitakuja na mwarobaini wa mafanikio yako (tena hakuna yeyote mwenye mwarobaini wa mafanikio yako). Nitakachofanya mimi ni kukushauri mbinu za kiujumla na siri za kufanya biashara. Lakini ukitaka tija zaidi nitakupa wazo jingine.

Kwa mfano; kama wewe ni mfanyabiashara wa huduma za daladala ama unakusudia kuanzisha biashara hiyo ni vema ukamtafuta mfanyabiashara mzoefu katika eneo hilo la daladala ili akupe ‘specific’ mbinu na mazingira halisi. Huyu kwako mimi ninamhesabu ni mtaalamu wako. Itakuwa ni bahati tu inapotokea umeniomba ushauri wa kibiashara halafu ikawa kuwa biashara unazofanya ama kukusudia kufanya ni zile ambazo mimi pia ninazifanya.

Maana yangu hapa ni kuwa, utaalamu katika biashara upo wa aina mbili. Kuna wale waliokaa darasani na kufundishwa biashara (bila kujali ikiwa wanafanya ama hawafanyi biashara) na wengine ni wale ambao licha ya kutoingia darasani, wanauzoefu mkubwa wa kibiashara. Hawa wote ni vema kuwatumia kwa kadiri ya mazingira na mahitaji yako kibiashara.

Unapotafuta mtaalamu wa kukushauri (ikiwa unataka msomi) mimi ninadhani ni vema kuwapata wataalamu ambao wana uzoefu wa kivitendo katika biashara mbalimbali.Robert Kiyosaki, katika kitabu chake cha “Guide to Investing” anashauri kuwa “ukitaka kwenda kupanda mlima Evarest, ni vizuri ukamuuliza mtu aliyewahi kupanda mlima Evaresti”. Mimi ninaongeza hapa kwa kusema, ukitaka kwenda hifadhi ya Ruaha, muulize mtu aliyewahi kwenda huko. Pia katika biashara ni vizuri kupata ushauri kwa wafanya biashara walio ktika biashara.

Najua hii ni changamoto kubwa kwa sababu wasomi wengi wa mambo ya biashara hawafanyi biashara, lakini kwa kuwa tunao wasomi wachache wa biashara ambao wanafanya biashara ni vema kuwatumia hao. Bila kuwa makini unaweza kupotezwa kwa sababu ‘wataalamu’ wengi hutumia muda mwingi kueleza namna mambo yasivyowezekana.

Hata hivyo katika ufanyaji biashara, ni vema sana kuachana na mazoea ya kufanya biashara kienyeji, badala yake kuna umuhimu wa kuingiza utaalamu katika ujasiriamali wetu. Hii itasaidia sana kuratibu mafanikio yako na kuachana na hesabu za kubahatisha kwa kwenda kwa kupapasa.Tunapaswa kuwatumia wataalamu washindi katika biashara zetu.

meshackmaganga@gmail.com

Aliyetangaza Kujinyonga Kwa Kiingilio Amehairisha Kutekeleza Zoezi Hilo

Katika mazingira ya kutatanisha aliyewahi kuwa mfanyabiashara maarufu mkoani Iringa Bwana Makosa alitangaza kujinyonga katika tukio ambalo alidai atalifanya hadharani na atayetaka kushuhudia atalipia kiingilio ambacho kwa mujibu wake kingesaidia familia yake na watoto yatima. Mjengwa Blog ilimtafuta ili kujua kwanini ameamua kufanya hivyo na afikirii kama kufanya hivyo ni kwenda kinyume na sheria za jamhuri na hata katika vitabu vya dini jambo hilo ni dhambi kubwa maana mwenye mamlaka juu ya kuchukua uhai wa mtu ni yule aliyetoa uhai ambaye sote tunaamini ni Mungu mmoja aliye juu mbinguni, Sasa kwanini Makosa ameamua kufanya hivi? ifuatayo ni Execlusive Interview fupi kati ya mdau wa Mjengwa Blog Na Makosa ambayo ilibidi ifanyike baa maana sikuwa na Miadi naye kwahiyo ilikuwa ni ghafla tu
Mdau:Je ni lini unatarajia kutimiza lengo lako la kutaka kijinyonga?
Makosa: Embu nichukulie kiroba kwanza
Mdau: Kwahiyo nikikununulia kiroba kitakuwa ndio kiingilio changu siku ambayo utajinyonga?
Makosa:Sijinyongiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
Mdau: Kwahiyo umehairisha zoezi la kujinyonga ?
Makosa:Sijinyongiiiiiii
Baada ya hapo makosa akaanza kinipa Free style yaani alikuwa ananiimbia nyimbo aliyoniambia anataka kwenda kuirekodi hivyo akaniomba ushauri ni studio gani anaweza kwenda.
Mdau: Nadhani kwa jinsi unavyoimba ukienda kwa Marco Chali ataitendea haki nyimbo yako
Nikamwambia kama anaweza kuimba kidogo labda naweza kuwa meneja wake nikivutiwa na kipaji chake
Pata ladha ya mistari ya wimbo wa Makosa
Makosa: "Watoto wangu wana miiili midogo dogo ila wana Sauti" KUBWAAA, mke wangu anamwili mdogo mdogo mdogo ila ana mat*** MAKUBWAA, Toka siku nyingi mimi marafiki zangu ni watu "WAKUBWAA,
Mdau: Inatosha inatosha nimekubali kweli we ni mtu mkubwaaa ha ha ha ha
Wadau wa blog hii hiyo ilikuwa execlusive interview kati yangu na Jamaa aliyetangaza kujinyonga kwa kiingilio je mdau unaweza kumuweka katika kundi gani?

Wednesday, July 25, 2012

.Rais wa Ghana John Attah Mills afariki

Rais wa Ghana John Atta Mills amefariki ghafla wakati akipata matibabu.
Taarifa kutoka afisi ya rais zinasema kuwa alifariki ghafla baada ya kupelekwa hospitali siku ya Jumatatu usiku.
Msaidizi wake pia amethibitisha kufariki kwa kiongozi huyo.
Kifo cha rais wa taifa la pili duniani kwa ukuzaji wa cocoa kimekuja wakati alikuwa anajiandaa kupogania tena urais.
Rais Attah Mills ambaye husafiri mara kwa mara kwenda ng'ambo kwa matibabu alifariki muda mfupi baada y kupelekwa katika hospitali moja mjini Accra , Ghana.
Ni hivi majuzi tu rais huyo alisafiri hadi Marekani kwa kile kilichosemekana kwa ni uchunguzi wa kawaida wa afya yake.
Kwa muujibu wa katiba ya Ghana, Makamu wa Rais John Dramani Mahama anatarajiwa kushikilia hatamu za uongozi hadi uchaguzi wa urais utakapofanywa.
Ghana ilikuwa inatarajiwa kwenda katika uchaguzi mkuu mwezi Disemba mwaka huu ambapo John Attah Mills alikuwa ametangaza nia yake ya kutetea uadhifa wake.
Wakati wa uongozi wake, uchumi wa Ghana uliimarika na demokrasia kupanuka zaidi.
" Ni kwa masikitiko makuu na kwa moyo mzito... Tunatangaza kifo cha ghafla cha rais wa jamhuri ya Ghana " taarifa iliyotumiwa shirika la Reuters kutoka ofisi ya rais ilisema.
Tarifa hiyo ilisema kuwa Rais Mills mwenye umri wa miaka 68 alifariki saa chache tu baada ya kupelekwa hospitali.
Hata hivyo hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.
Lakini msaidizi wake mmoja ambaye hakutaka kutajwa, alisema kuwa Rais John Attah Millis alisikika siku ya Jumatatu akilalamika kwa anaumwa.
Hali yake ilizorota na hatimae kufariki mapema siku ya Jumanne.
Mills , anajulikana kwa kuanzisha uchimbaji wa mafuta nchi Ghana.

Monday, July 23, 2012

Marekani yaikatia Rwanda msaada wa kijeshi

Washington inasema itazuia msaada wa dolla laki mbili ambao ungesaidia idara ya mafunzo ya kijeshi Rwanda

Marekani imekata msaada wake wa kijeshi kwa Rwanda kutokana na wasiwasi kuwa serikali ya Kigali inaunga mkono waasi katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema ina ushahidi kuwa Rwanda inasaidia makundi ya waasi wa Congo, ikiwa ni pamoja na kundi la M23. Imesema itazuia msaada wa dolla 200,000 ambazo zilikuwa ziende katika idara ya mafunzo ya kijeshi ya Rwanda. Serikali ya Rwanda mara kwa mara imekanusha kusaidia waasi wa DRC.

Hatua ya Washington imekuja wiki moja baada ya marais wa Rwanda na DRC kukubaliana kuhusu kupelekwa kwa jeshi la kimataifa kupambana na waasi mashariki mwa Congo na kulinda doria katika mpaka unaounganisha nchi hizo.

Majeshi ya Congo yamejaribu kwa miaka kadha, bila mafanikio, kuzima makundi ya waasi katika eneo hilo lenye utajiri mkubwa wa madini.

Kundi la M23 linaundwa na wanajeshi wa zamani inaoaminika kuwa ni wafuasi wa Bosco Ntaganda, mbabe wa kivita anayetafutwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu kwa madai ya uhalifu wa wakati wa vita.

Matajiri waficha fedha ng'ambo

Utafiti mpya uliofanywa sehemu mbali mbali za dunia, kutaka kujua wapi watu wanaficha fedha zao kukimbia kodi, umegundua kuwa dola kama trilioni 20, zimefichwa nchi za ng'ambo, mbali ya macho ya maafisa wanaotoza kodi.
Ripoti hiyo imeandikwa na shirika la utetezi, Tax Justice Network, ambayo inasema kuwa tofauti baina ya matajiri na maskini ni kubwa kuliko ilivofikiriwa.
Dola trilioni 21 ni sawa na pato la mwaka la Marekani nzima pamoja na Japani.
Tax Justice Network inafikiri fedha zilizofichwa ng'ambo zinaweza kuwa zaidi ya hizo.
Ripoti yao inaonesha jinsi matajiri wakubwa wanavohamisha fedha na kuziweka kwenye nchi zinazoweka siri, kama Uswiswi na Visiwa vya Cayman, kwa kupitia mabenki ya kibinafsi.
Ripoti piya inaeleza kuwa nchi zenye utajiri wa mafuta, kama Urusi na Nigeria, ndio hasa kwenye mtindo wa fedha kutoweka na kuvushwa, badala ya kuwekezwa nchini.
Utafiti huo unamaliza kwa kusema wanasiasa sehemu mbalimbali za dunia, wanategemea kuwa fedha hata zikiwa kwa watu wa juu, zitavuja hatimae na kuwafikia maskini - ripoti inasema hayo hayatokei tena.

Friday, July 20, 2012

Marekani kukabiliana na Syria bila UN

Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Bi , Susan Rice, amesema Marekani itaimarisha juhudi zake nje ya baraza la usalama la Umoja wa Mataifa ili kushinikiza serikali ya Syria kuachia madaraka.
Bi. Rice, aliyasema hayo baada ya Urussi na Uchina kutumia kura zao za turufu katika baraza hilo la Usalama kupinga vikwazo zaidi dhidi ya serikali ya Syria, ikiwa haitasitisha utumizi wa silaha nzito nzito dhidi ya waasi na raia.

Urussi ilisema kuwa azimio hilo la baraza la usalama lililoungwa mkono na mataifa ya Magharibi halikubaliki kwa sababu lingetekelezwa kwa kuwatumia wanajeshi.
Msemaji wa mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Syria, Kofi Annan, Ahmad Fawzi, alisema Bwana Annan, amesikitishwa sana na hatua hiyo ya Urussi na Uchina ya kutumia kura zao za turufu kupinga azimio hilo.
Wakati huo huo wapiganaji wa upinzani nchini Syria wameuteka na kutwaa uthibiti wa vituo kadhaa vya kuvuka mpaka kuingia nchini Iraq na Uturuki.
Naibu waziri wa mambo ya ndani wa Iraq, amesema wapiganaji wa waasi wa Free Syrian Army, wametwaa uthibiti wa kituo kinachotumiwa kuingia nchini humo kutoka Syria.
Katika kituo kingine cha mpakani nchini Iraq, maafisa wa serikali ya nchi hiyo wamesema wanajeshi wa waasi wamewauawa takriban wanajeshi 20 wa serikali ya Syria.
Kituo muhimu cha kuingia Uturuki kutoka Sria cha Bab al Hawa pia kilitwaliwa na waasi hao, lakini wameanza kuondoka.

Wednesday, July 18, 2012

National Forces Alliance chashinda Libya

Chama cha National Forces Alliance, kinachoongozwa na aliyekuwa Waziri Mkuu wa mpito Mahmoud Jibril kilipata ushindi kwa kunyakua viti 39.
Chama cha mwelekeo wa Dini ya kiislamu cha Muslim Brotherhood kilichukua nafasi ya pili kwa kushinda viti 17.
Bunge hilo la wanachama 200 litakuwa na wabunge wengi wa kujitegemea.
Bunge hilo litakuwa na mamlaka makubwa ambapo linatarajiwa kuunda Serikali mpya ya mpito na wakati huohuo kusimamia shughuli za kutunga Katiba mpya.
Wabunge hao wanapaswa kushikilia madaraka yao kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Nao Raia wa libya wana matumaini kuwa uchaguzi huo ni mwanzo mpya wa utaratibu wa utawala wa kidemokrasia nchini.

Monday, July 16, 2012

20 Percent: Afande Sele kachanganyikiwa

Uswahiba kati ya wasanii wawili wa Bongo Flava nchini, Afande Sele na 20 Percent umeingia dosari baada ya kutupiana maneno kila mmoja kwa nyakati tofauti kwenye vyombo vya habari.
Maneno hayo yalianza wiki iliyopita baada ya Afande Sele kuzungumza na Clouds FM na kudai kusikitishwa na kitendo cha swahiba wake 20 Percent cha kugoma kutumbuiza kwenye tuzo za muziki za Zanzibar wakati alikuwa amelipwa pesa zote.
Kufuatia mgomo huo, waandaaji walimpeleka lock-up msanii huyo na kubaki na laptop yake mpaka pale atakapowarudishia waandaji hao shilingi milioni moja waliyompa kwaajili ya kuperform kwenye tuzo hizo.
Hatimaye jana 20 Percent alizungumza na kituo hicho cha radio kuhusiana na tukio lenyewe na kusema kuwa Afande Sele amechanganyikiwa na anasumbuliwa na njaa ndio maana anamlaumu.
Akiongea kwa jaziba, 20 Percent amesema Afande Sele ni kama ‘mtoto’ na alimshangaa kufahamu kuwa alifika Zanzibar saa sita usiku bila kuwa sehemu ya kulala kutokana na waandaaji hao kuwa wababaishaji.
Amesema waandaji wa tuzo hizo ni ‘wahuni’ tu ndo maana alikataa kuperform na kuongeza kuwa maisha yake hayategemei muziki wa Bongo Flava.
Kuhusu Laptop yake iliyobaki kwenye mikono ya waandaji wa tuzo hizo, msanii huyo wa ‘Tamaa Mbaya’ amesema hatoifuata Zanzibar bali watampelekea wenyewe.
Miaka ya hivi karibuni, Afande Selena 20 Percent walionekana kuwa maswahiba wa nguvu lakini tukio hilo linaonesha kuutulia doa ushkaji wao.

MAKOSA: NIPO TAYARI KUFA KWA KUJINYONGA

Aliyekuwa mfanyabiashara mkubwa mjini Iringa Bw Makosa anadai yupo tayari kufa dunia imemshinda

Mfanyabiashara maarufu ambaye kwa sasa amefulia vibaya Bw Makosa (kushoto) akizungumza na mtandao huu kuhusu hatua yake ya kukusudia kuandaa tamasha kubwa katika uwanja wa Samora ambako watu wataingia kwa kiingilio ili kujinyonga na fedha hizo zisaidie kulea familia yake.CHANZO:http://francisgodwin.blogspot.com/ 


Mubarak kurejeshwa jela

Mwendesha mashtaka mkuu nchini Misri, ameaumuru rais wa zamani wa nchi hiyo, Hosni Mubarak kurejeshwa gerezani akisema kuwa hali yake ya afya imeimarika sasa. Mubarak, mwenye umri wa miaka ,84, alihamishwa kutoka gerezani humo mwezi jana baada ya ripoti za afya yake kuzorota .

Alisemekana wakati huo kuwa alipatwa na kiharusi mwa mpigo na kuwekwa kwenye mashine ya kupiga moyo. Ripoti za Mubaraka kupoteza fahamu wakati huo zilipingwa vikali.

Mwezi Juni , Mubarak alihukumiwa kifungo jela baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya waandamanaji waliokuwa waanpinga utawala wake.

Mkuu huyo wa mashtaka, Abdel Maguid Mahmoud alitoa agizo la kumhamisha rais Mubaraka kutoka hospitali ya kijeshi ya Maadi hadi katika hospitali ya Tora baada ya afya yake kuimarika.

Naibu wa Mahmoud, Adel al-Saeed, ilisema kuwa jopo la madaktari lilikuwa hapo awali limesema kuwa afya ya rais huyo wa zamani iko sawa sasa mradi atumie madawa yake na kwamba kwa mtu mwenye umri wake hilo ni sawa.

Hata hivyo haikujulikana mara moja lini Mubaraka atarejeshwa tena gerezani.

Aidha mwandishi wa BBC mjini Cairo anasema kuwa taarifa zozote kuhusu afya yake, wamisri wanazichukua kwa shauku kubwa.

Kumekuwa na shauku kubwa kuhusu afya ya Mubarak wengi wakisema kuwa taarifa zozote kuhusu afya ya Mubarak zinatafsiriwa kama njama ya yeye kutaka kutolewa gerezani kwa misingi ya afya yake.

Hata hivyo wengi wanajua kuwa huu sio mwisho wa wao kusikia kuhusu sakata hii ya afya ya Mubarak.

Sunday, July 15, 2012

Clinton amzuru Mursi Misri

Waziri wa mashauri ya Nchi za Nje wa Marekani, Hillary Clinton, yuko nchini Misri kukutana na kiongozi mpya, rais kutoka chama cha muslim brotherhood, Mohamed Morsi.

Miaka iliyopita, waziri mmoja wa mashauri ya nchi za nje wa Marekani, alitangaza Marekani haizungumzi na muslim brotherhood, na daima haitafanya hivo.


Sasa, serikali ya Rais Obama, imefanya haraka kuwasiliana na rais mpya wa Misri wa muslim brotherhood, Mohamed Morsi.

Marekani imekubali kuwa ukweli hauepukiki, na inajaribu iwezavyo.

Bila ya shaka Hillary Clinton atataka kupata ahadi ya Rais Morsi, juu ya siasa za Misri kuhusu mambo ya nje na ya ndani ya nchi.

Serikali ya Marekani inataka kuona demokrasi na haki za kibinaadamu zinalindwa nchini Misri.

Kwa upande wao, muslim brotherhood wamesisitiza mara kadha kwamba hawataki kutengwa na ulimwengu, hasa kwa sababu nchi hiyo inategemea sana biashara za kimataifa na utalii.

Saturday, July 14, 2012

Mwandishi afungwa jela miaka 18 Ethiopia

Mwanahabari maarufu ambaye pia ni mwandishi wa Blogi amefungwa jela miaka 18 nchini Ethiopia kwa madai ya kukiuka sheria ya ugaidi.
Eskinder Nega na wenzake 23 walipatikana na hatia mwezi uliopita.
Walikamatwa kwa madai ya kuwa na uhusiano na kundi moja la upinzani lililo na makao yake Marekani kwa jina Ginbot Seven.
Serikali ya Ethiopia inadai kuwa kundi hilo ni la kigaidi.
Mahakama hiyo ya Addis Ababa pia ilimfunga jela maisha mwanaharakati wa upinzani,Andualem Arage.
Kutokana na kazi yake ya uwana-habari na kuandika Blogi, Mwezi wa May, Eskinder alipewa tuzo maarufu la kimarekani la Pen America's Freedom to Write.
Makundi ya kutetea haki za kibinadamu zimekuwa ikiilaumu serikali kwa kubuni sheria hiyo ya kukabiliana na ugaidi yakisema sheria hiyo haifai.
Siku ya Ijumaa Mwanahabari ,Eskinder na mwanachama wa chama cha upinzani cha Unity for Democracy and Justice party walikuwa mahakamani kuhukumiwa.
Washukiwa wengine 16 waliopatikana na hatia mwezi wa Juni wako ukimbizini.
Walipokuwa wakiingia mahakamani wawili hao waliwapungia mikono jamaa zao na marafiki pamoja na maafisa wa kibalozi waliokuwemo ndani.
Eskinder alikamatwa mwezi wa Septemba mwaka jana baada ya kuandika makala iliyokuwa ikiilaumu serikali ya Ethiopia kwa kukamata wapinzani wake kwa kutumia sheria ya ugaidi.
Miongoni mwa watu ambao wamekamatwa chini ya sheria hiyo ni msanii na mcheza filamu maarufu nchini Ethiopia, Debebe Eshetu ambaye ni mkosoaji mkuu wa serikali.

Thursday, July 12, 2012

Binti Amuua Baba yake kisa Boyfriend

PAKISTAN: The father of a girl who was not happy with his daughter's boyfriend paid with his life for airing his views.

The teenage daugter of the man from Pakistan's Punjab province killed her father for scolding her over the choice of her boyfriend, reports news agency Press trust of India.
According to neighbours, the boyfriend had been causing a lot of trouble in the father-daughter relationship as the father was against the relationship and had even beaten his daughter to conform to his wishes.
However, the beating only turned the daughter more against her father. She asked her boyfriend to give her a gun and she used the weapon on her father while he was asleep.
The girl was arrested by the police and her boyfriend was also charged with abetment to murder