Chama cha soka mkoa wa Iringa ( IRFA) kimeeleza sababu ya timu ya vijana wa
mkoa wa Iringa iliyoshiriki Copa Cocacola kutolewa mapema katika mashindano hayo
kuwa ni kutokana na mwamko mdogo wa wakazi wa mkoa wa Iringa .
Katibu mtendaji wa IRFA Eliud Mvella Wamahanji ametoa kauli hiyo Leo katika
ukumbi wa VETA mjini Iringa wakati wa kumpongeza aliyekuwa katibu mkuu wa
shirikisho ya mpira wa miguu nchini ( TFF) Frederick Mwakalebela ambaye
amejitolea kuwa mdhamini mkuu wa mashindano ya wilaya ya FA wilaya (Mwakalebela
Cup 2012)
Wamahanji alisema kuwa mbali ya Mwakalebela kujitolea kuwa mdhamini katika
mashindano hayo ila ndie aliyejitolea awali kusaidia jezi timu hiyo ya Copa
Cocacola ila zaidi yake hakuna hata mdau mmoja ambaye amejitolea kusaidia timu
hiyo.
Aidha Wamahanji alisema kuwa pamoja na jitihada mbali mbali ambazo IRFA
imekuwa ikizifanya katika mkoa wa Iringa kuendeleza michezo ila bado wapo baadhi
ya watu ambao ni wakazi wa mkoa wa Iringa wamekuwa ni mabingwa wa kusemamea
vibaya mkoa badala ya kusaidia .
Hata hivyo alionya tabia ya baadhi ya watu mkoa wa Iringa kuendesha
mashindano kinyume na taratibu na kanuni za soka kwa kuchezesha mashindano bila
haraka za TFF .
Awali mwenyekiti wa Chama cha soka Manispaa ya Iringa ( IMFA) Ramadhan
Mhano alitaja timu ,ambazo zitashiriki katika mashindano hayo FA Mwakalebela Cup
ni pamoja na Mkwawa FC, Lipuli FC, BBC FC, Real moja FC ,Don Bosco FC, Magereza
FC ,Mlandege FC, Ruaha FC,Uhuru FC, Sengo FC,Nyota Njema FC, Mshindo FC,Young
stars FC na Upendo FC.
|
No comments:
Post a Comment