Monday, October 14, 2013

Dk Slaa arejea Tanzania baada ya kumaliza ziara nchini Marekani

zzzw.slaaorig_eb0cb.jpg
Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Dk Wilbrod Slaa leo Jumapili 13 Oktoba amesafiri kurudi Tanzania baada ya ziara yake iliyomchukua wiki tatu nchini Marekani.
Dk Slaa aliwasili nchini Marekani tarehe 21 Septemba 2013 akiambatana na mkewe mama Josephine Mushumbuzi na kupokelewa na Uongozi wa Chadema DMV.
Tarehe 22 Septemba 2013 Dr Slaa alifanya mkutano uliojumuisha wanajumuia ya Watanzania waishio katika Majimbo ya Washington, Maryland na Virginia.(P.T)
Katika ziara yake Dk Slaa alitembelea majimbo ya North Carolina na Alabama ambako alitembelea Vyuo Vikuu na Taasisi mbalimbali na kujifunza Shuguli nyingi za Maendeleo katika Sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo, Afya, Nishati na Uchumi.
Akizungumza akiwa uwanja wa Ndege wa Dulles mjini Washington Dk Slaa alisema alichojifunza akiwa Marekani anatarajia kupeleka maarifa hayo Tanzania ili yaweze kumkomboa Mtanzania kutoka katika Umaskini. Moja katika mambo ambayo amejifunza ni namna ya kutumia nishati ya Jua kuzalisha umeme hasa kwa wakazi wa Vijijini.
Dk Slaa amekamilisha ziara yake ya wiki tatu nchini Marekani iliyopewa jina la "Vision Tanzania" baada ya kualikwa na Umoja wa Vyuo vikuu nchini Marekani.
Taarifa hii imetolewa na waratibu wa CHADEMA Blogs

Sunday, October 13, 2013

Utalii umeingiza Trilioni ngapi kwa Tanzania? Idadi ya watalii je?


Utalii 2  Unaambiwa Utalii nchini Tanzania kwa mwaka 2012 peke yake umeingiza shilingi Trilioni 2.69 kwenye pato la taifa ikiwa ni ongezeko la asilimi 24 ikilinganishwa na mwaka 2011.
Jingine la kufahamu ni kwamba, Watalii wanaotembelea Tanzania kutoka nje ya nchi idadi yao imekua ikiongezeka kila mwaka kutoka Watalii laki nane na elfu 67,994 mwaka 2011 mpaka milioni moja na elfu sabini na saba 58 mwaka 2012.
Philiph Chitaunga ambae ni meneja wa huduma za utalii kutoka bodi ya utalii Tanzania amesema sasa hivi kuna mpango maalum kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko Tanzania.

www.millardayo.com

MBIO ZA MWENGE WA UHURU ZAMALIZIKA ,MKOA WA IRINGA WAKABIDHI TAIFANI ASUBUHI YA LEO

 Mwenge  wa uhuru  ukiwasili katika uwanja wa  kilele  cha mbio za mwenge kitaifa  uwanja wa Samora  ukitokea  viwanja  vya mkesha  Mwembetogwa ambako ulikesha kwa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa
 Viongozi  wa  serikali ya mkoa wa Iringa na  wananchi wakisubiri kupokea mwenge  kutoka Manispaa ya Iringa  leo
 Ulinzi  mkali uwanja  wa samora  leo
 Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Dr Christine Ishengoma kulia akipokea  mwenge  kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Iringa Dr Leticia  Warioba baada  ya Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa kumaliza mbio  hizo kwa kuzindua miradi 8  yenye thamani ya Tsh milioni 940.2
 Mkuu  wa  mkoa  wa Iringa Dr Ishengoma  akiwa amepokea mwenge  huo tayari kluukabidhi Taifa
 Viongozi wa Kitaifa  wakiongozwa na waziri wa habari vijana utamaduni na michezo Dr Fenela Mkangala wa  tatu  kulia  wakisubiri  kukabidhiwa mwenge leo  uwanja wa samora
 Mkuu  wa mkoa  wa Iringa Dr Ishengoma akisoma taarifa ya miradi iliyopitiwa na mbio za mwenge mwaka 2013
 Mkuu wa mkoa  wa Iringa Dr Ishengoma  akijiandaa kumkabidhi mwenge  waziri Dr Mkangala  leo uwanja  wa Samora
 Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma kulia akimkabidhi mwenge wa uhuru waziri Dr Mkangala  leo  uwanja  wa Samora kabla ya  waziri  huyo kuukabidhi mwenge  huo kwa vijana ili kuja kuukabidhi kwa rais Dr Kikwete kwa kuuzima mapema leo

 Waziri Dr Mkangala  akivipongeza  vyombo vya ulinzi mkoa  wa Iringa
 kamanda  wa polisi mkoa  wa Iringa  Ramadhan Mungi kulia akimpongeza mkuu wa FFU mkoa wa Iringa S.A Mnunka kwa kazi nzuri ya kukimbiza mwenge  vizuri mkoa wa Iringa



Waziri Dr Mkangala kulia akiwa na viongozi wa mkoa  wa Iringa  leo

Chanzo: www.matukiodaima.com

Monday, September 23, 2013

Milio ya risasi yasikika ndani ya Westgate

Huku hali ya mshikemshike ikiendelea kushuhudiwa katika jengo la Westgate lenye maduka, ufyatulianaji risasi umesikika ndani ya jengo hilo lenye maduka na mikahawa zaidi ya themanini.


Wapiganaji wa Al shabaab wamewateka nyara raia ambao idadi yao haijulikani. Walikuwemo ndani ya jengo wakiendelea na shughuli zao kuanzia Jumamosi mchana wakati wapiganaji wa Al shabaab walipowavamia na kuanza kufyatua risasi kiholela.

Inaarifiwa kuna maiti kumi katika ghorofa ya kwanza ya jengo hilo.


Inaarifiwa wapiganaji hao wanaoaminika kuwa wanachama wa Al Shabaab ni kati ya kumi na kumi na watano na bado wangali ndani ya jengo hilo.


Ripoti zinasema kuwa ufyatulianaji mkubwa wa risasi umesikika katika jengo hilo kwa takriban dakika 15.

Harakati za kuendelea kumaliza operesheni hiyo zinaendelea lakini hali ya mateka walio ndani ya jengo hilo inaendelea kudorora.


Wakenya waliofanikiwa kuondoka katika jengo la Westgate kwa usaidizi wa polisi

Rais Kenyatta amesema kuwa jueshi linajitahidi kuhakikisha kuwa linakabiliana vilivyo na wanamgambo hao.

Helikopta za polisi zinazunguka juu ya jengo hilo pamoja na ndege za kijeshi kushika doria. Vikosi vya usalama vinaendelea na operesheni kujaribu kuwanusuru waathiriwa wakati hali ikiwa ni ya ati ati katika eneo la shambulizi.


Awali jeshi la Kenya lilisema limeweza kudhibiti jengo hilo lote ingawa bado limetaja hali kuwa tete mno hasa katika kujaribu kuwaokoa mateka waliosalia ndani ya jengo hilo.


Ripoti zinasema kuwa watu 69 wamefariki katika shambulizi hilo la Al Shabaab kufikia sasa huku 175 wakijeruhiwa. Baadhi wametibiwa na kuondoka hospitalini. Baadhi ya majeraha waliyopata ni majereha ya risasi na kutokana na guruneti ambalo Al shabaa waliwarushia wale waliokuwa ndani ya mikahawa siku ya Jumamosi.


Kundi hilo limekiri kutekeleza shambulio hilo kutokana na hatua ya kenya kupelekeka majeshi yake nchini Somalia ili kukabiliana na wapiganaji hao.

http://www.bbc.co.uk


Friday, September 20, 2013

WAZIRI KABAKA AZINDUA RASMI MCHAKATO WA MAANDALIZI YA USHIRIKI WA WAJHASIRIA MALI

Waziri wa Kazi na Ajira  Mhe. Gaudentia  Kabaka  leo  tarehe  19/09/2013, amezindua  rasmi  mchakato wa  maandalizi ya ushiriki wa Wajasiria mali wa Tanzania  katika Maonesho ya 14 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yajulikanayo  kama  Nguvu kazi/Jua kali.

Maonesho hayo yaliyoanza kufanyika  mwaka  1999 jijini Arusha  Tanzania wakati wa kusainiwa mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yameendelea kufanyika kila mwaka kwa mzunguko katika nchi ya wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Dhumuni kuu la maonesho haya ni kuwezesha sekta  isiyo rasmi kukua na kurasimisha shughuli zao katika ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuwapatia fursa Wajasiriamali wa sekta hii kuonesha bidhaa zao, kukutana na wenzao, kubadilishana taarifa, ujuzi, kukuza masoko ya bidhaa na huduma pamoja na kuwezesha kupanuka kibiashara.

Jumla ya Wajasiriamali 1,070 kutoka nchi tano za  Jumuiya ya Afrika Mashariki wanategemewa kushiriki na Tanzania inatarajiwa kupeleka washiriki 250.

Mhe. Waziri Kabaka amesema,ili kurahisisha na kuharakisha ushiriki wa Wajasiriamali wa Tanzania katika maonesho hayo, kuna swala la usajili, na fomu za usajili pamoja na vigezo vya kuangalia kabla ya kujaza fomu ambavyo vinapatikana kwenye  Tovuti ya Wizara ambayo  ni www.kazi.go.tz

IMETOLEWA
Ridhiwan.M.Wema
Msemaji
WIZARA YA KAZI NA AJIRA.
19/09/2013

Hakimu achomwa kisu mahakamani


Wauguzi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga wakimuhudumia hakimu Satto Nyangoha aliyechomwa kisu shavuni jana, akiwa mahakamani na mlalamikaji katika kesi ya wizi wa baiskeli, Emmanuel Izengo. Picha na Suzy Butondo
Shinyanga. Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo iliyopo eneo la Nguzo Nane, Kata ya Kambarage Mjini Shinyanga, Satto Nyangoha amejeruhiwa kwa kuchomwa kisu katika shavu lake la kushoto baada ya kutoa hukumu ya kesi ya wizi wa baiskeli.
Kitendo hicho kinadaiwa kufanywa na mlalamikaji katika kesi hiyo, Emmanuel Izengo (28), mkazi wa Tambukareli, Shinyanga baada ya kutokuridhishwa na hukumu iliyotolewa bila ya mshtakiwa, Daniel Makelezia, mkazi wa Lubaga Shinyanga na mdhamini wake, Marko Nkelezia kuwepo mahakamani.
Katika hukumu yake, Hakimu Nyangoha alisema mshtakiwa atakapopatikana atatumikia kifungo cha miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa baiskeli hiyo aina ya Neria yenye thamani ya Sh150,000.
Awali, ilielezwa kwamba baada ya tukio hilo la wizi lililotokea Agosti Mosi, mwaka huu katika eneo la Nguzo Nane, mshtakiwa alikamatwa na kuwekwa mahabusu na kufunguliwa kesi namba 460 ya 2013 kabla ya kuachiwa kwa dhamana Agosti 23, mwaka huu huku kesi yake ikiendelea na pande zote mbili zilitoa maelezo.
Hata hivyo, baada ya kutoa maelezo, si mshtakiwa wala mdhamini wake aliyehudhuria mahakamani hapo licha ya kesi hiyo kusikilizwa mara mbili bila ya taarifa yoyote kabla ya hakimu huyo kutoa hukumu hiyo jana.
Kushambuliwa
Baada ya hukumu hiyo mlalamikaji alitoa shukrani na kuwashika mikono wote waliokuwamo mahakamani humo na kutoka nje.
Ilidaiwa kuwa baada ya dakika 15, Izengo alirudi mahakamani hapo na kudai kuwa ameleta risiti ya kumwonyesha hakimu thamani ya baiskeli yake alipoingia ndani ndipo kelele za Mshauri wa Baraza, Mary Wamba zikaanza kusikika akisema: ‘Njooni jamani hakimu kavamiwa anapigwa’.
Baada ya watu waliokuwa karibu kuingia katika ofisi ya Mahakama hiyo walikuta hakimu ameshacwhomwa kisu katika shavu la upande wa kushoto huku akivuja damu nyingi huku mtuhumiwa huyo akiendelea kumshambulia. Baada ya tukio hilo, wasamaria wema walimpeleka hakimu huyo katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga ambako alilazwa kwa matibabu.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Evarist Mangala alisema mtuhumiwa alikamatwa mara baada ya tukio hilo kusubiri hatua za kisheria dhidi yake.
http://www.mwananchi.co.tz/

Polisi wakosoa uchunguzi wa Marikana



Polisi nchini Afrika Kusini wameikosoa tume inayochunguza mauaji ya wafanyakazi thelathini na nne katika mgodi wa madini ya platinum huko Marikana Agosti mwaka uliopita kusema kuwa walidangaya.
Katika taarifa idara ya polisi imesema kuwa madai dhidi yao ni ya kuudhi na hayana msingi.
Mawakili katika tume hiyo ya Marikana wamelaumu polisi kwa kutoa ushahidi wa uongo kuhusu hatua ya kutumia risasi wakitaka ukubalike bila upinzani.Wamesisitiza kuwa walitumia risasi kujilinda walipokuwa wakijaribu kuwatawanya na kuwapokonya silaha wafanyikazi hao waliokuwa wakigoma.

Baada ya kuchunguza kwenye Kompyuta za polisi walisema kuwa polisi walikuwa wamezuilia na kubadilisha yaliyokuwemo katika stakabadhi hizo.
Tume hiyo kwa mara nyingine imeakhirisha vikao vyake inapopitia maelfu ya stakabadhi zinazohusiana na tukio hilo.
Sasa polisi wanasema kuwa wamekuwa wakishirikiana na tume hiyo ya Marikana kikamilifu bila vikwazo vyovyote. Kadhalika wanataka wapewe nafasi kujieleza kabla ya mawakili kutoa hukumu.
http://www.bbc.co.uk/swahili

87 WAUAWA NA BOKO HARAM NIGERIA

tahmasebi20130917235522900_0a797.jpg
Wapiganaji wa Boko Haram wamewaua watu 87 katika shambulio katika Jimbo la Borno nchini Nigeria.
Mashahidi wanasema kuwa wapiganaji hao waliteketeza nyumba kadhaa katika tukio hilo la kutisha mnamo Jumanne usiku.
Shambulio hili limetokea siku chache baada ya makabiliano makali kati ya jeshi na wapiganaji wa Boko Haram
Wanamgambo hao waliokuwa wamevelia magwanda ya jeshi, waliweka vizuizi barabarani nje ya mji wa Benisheik na kuwapiga risasi wale waliokuwa wanajaribu kutoroka.(P.T)
Kwa mujibu wa taarifa za mashahidi , wapiganaji hao waliteketeza nyumba katika shambulizi hilo la Jumanne.
Kundi la Boko Haram, ambalo linapigania linachosema ni taifa la kiisilamu nchini Nigeria, limekuwa likifanya mashambulizi sawa na haya kuanzia mwaka 2009.
Jeshi linadai kuwa Agosti mwaka huu, kiongozi wa kundi hilo Abubakar Shekau na naibu wake Momodu Bama waliuawa , ingawa hakuna taarifa za kujitegemea kuthibitisha hilo.
Mawasiliano katika jimbo la Borno, yamekumbwa na hitilafu, tangu mwezi Mei, wakati hali ya hatari, ilipotangazwa katika jimbo hilo na majimbo mengine mawili.
Lakini mashambulizi yameongezeka sana hivi karibuni tangu jeshi kuanza kukabiliana na kundi hilo katika maeneo yaliyoathirika zaidi.

Tuesday, September 3, 2013

MNARA WA DAUD MWANGOSI HUU HAPA

601_n_c3006.jpg
Leo Nyololo kwenye uzinduzi wa mnara wa kumbukumbu ya mauaji ya Daudi Mwangaosi, Kulia ni Benson Kigaila,wapili kutoka kulia ni Mdogo wake marehemu mwangosi,anayefuata ni Winfrida,na wa kwanza kutoka kushoti ni naibu katibu mkuu,Chadema Zanzibar Hamad Yusuf.(P.T)
Kwa hisani ya Mjengwa Blog.

Monday, September 2, 2013

KUMBUKUMBU YA MAREHEMU DAUDI MWANGOSI , MAANDAMANO YA WANAHABARI YATIKISA MJI WA IRINGA


Wanahabari  wa  vyombo  mbali mbali na  wadau  wa habari  mkoa  wa  Iringa  wakiwa katika  maandamano ya amani ya  kumuenzi  aliyekuwa mwenyekiti  wa klabu ya  waandishi  wa  habari  mkoa  wa Iringa (IPC) leo 
Maandamano  ya  wanahabari na  wadau  wa  habari yakipita  eneo la soko kuu la manispaa ya  Iringa 
Katibu  wa IPC  Francis  Godwin  akiongoza  maandamano ya  wanahabari na  wadau huku akiwa  juu ya gari na picha ya marehemu Daudi Mwangosi
Wanahabari  Iringa katika maandamano ya  kumuenzi  marehemu  Mwangosi  leo
 Maandamano ya  wanahabari  na  wadau  wa habari  mkoa wa Iringa ya  kumuenzi marehemu Daudi Mwangosi  yakipita  eneo ya  uhindini  


 Wananchi  wakishuhudia maandamano  hayo  leo





Katibu  mtendaji  wa IPC  Francis  Godwin akitoa taarifa ya  kuanza kwa maandamano ya kumuenzi marehemu Daudi Mwangosi leo
Katibu  wa  IPC Francis  Godwin mwenye pama akikabidhi maandamano ya  mwenyekiti  wa IPC Frank Leonard na  wadau  wengine  eneo la Maktaba ya  mkoa wa Iringa


Katibu  wa  IPC  FrancisGodwin kushoto akikabidhi picha ya marehdemu Daudi Mwangosi kwa  mwenyekiti  wa IPC  Frank Leonard kulia,wanaoshuhudia ni mzee  Fulgence  Malangalila  na Majid Mjengwa 


Mwenyekiti wa  IPC Frank Leonard  kushoto akikabidhi  picha ya  Mwangosi kwa mwasisi  wa IPC mzee Fulgence Malangalila 









MAANDAMANO ya  wanahabari  mkoa  wa  Iringa  kwa  ajili ya  kumbukumbu  ya  mwaka  mmoja wa  kifo  cha  aliyekuwa  mwenyekiti  wa klabu ya  waandishi  wa habari  mkoa  wa  Iringa (IPC) na mwandishi  wa Chanel  Ten Marehemu  Daudi Mwangosi  yatikisa mji  wa  Iringa leo.

Maandamano  hayo ambayo  yameanza majira ya saa 4 asubuhi  katika  viwanja   vya  bustani ya  Manispaa ya  Iringa yamepata  kuzungukakatika maeneo  mbali mbali ya  mji wa  Iringa kabla ya  kupokelewa na mwenyekiti  wa IPC  Frank Leonard katika  ukumbi wa maktaba ya  mkoa kwa mkutano wa  wadau  wa habari.

katika  maeneo  mbali mbali  ambayo maandamano  hayo yamepita  likiwemo  eneo la Uhindini , Mashine  tatu, Soko  kuu na stendi  kuu ya mabasi ya mikoani  wananchi  walilazimika  kusitisha  shughuli  zao kushuhudia maandamano  hayo ambayo yaliongozwa na  askari  wa  usalama barabarani .

CHANZO: www.francisgodwin.blogspot.com