Saturday, August 16, 2014

Marekani yashambulia wapiganaji wa Iraq


Wapiganaji wa Islamic State wakidhibiti bwawa kubwa zaidi nchini Iraq
Ndege za kijeshi kutoka Marekani zimetekeleza mashambulizi tisa ya angani dhidi ya wanamgambo wa Islamic State kazkazini mwa Iraq ili kuvisaidia vikosi vya Iraq kuliteka bwawa moja muhimu karibu na mji wa Mosul.
Bwawa hilo ndio kubwa nchini humo na lilitekwa na islamic state mapema mwezi huu.
Makamanda wa Marekani wamesema kuwa mashambulizi hayo yalioanza ijumaa usiku yaliharibu zaidi ya magari 14 ya kivita yanayomilikiwa na Islamic State.
Duru mjini Mosul zimearifu kuwa takriban wapiganaji kumi na moja wanadaiwa kuuawa katika shambulizi hilo.
Jenerali mmoja wa vikosi vya Kikurdi kazkazini mwa Iraq amesema kuwa vikosi hivyo vimeanzisha mashambulizi ya kuliteka bwawa hilo

CHANZO: http://www.bbc.co.uk/swahili/habari

Sunday, June 8, 2014

Funza chakula kipya cha mifugo


 


Je unaweza kula nyama ya mifugo waliolishwa Funza? Kufuga Nguruwe, Kuku, Samaki kwa kuwalisha funza, kunatarajiwa kubadili tunavyo fuga mifugo.
Haya hufanyika katika sehemu moja ya kufanyia majaribio inayomilikiwa na kampunib ya AgriProtein nchini Africa Kusini.
Kampuni hiyo inatengeneza litakalokua shamba kubwa kabisa duniani , linalofuga Nzi. Ufaransa, Kanada, Uholanzi, na Marekani pia wana mipango hiyo.
Mamia ya watu walishiriki kikao cha 'Funza kulisha Ulimwengu' , kilichofanyika huko Wageningen, Uholanzi, mapema mwezi huu.
Wengi waliridhika kuwa Funza na Buu wanaweza kutupa lishe mbadala kwa lishe ile ya kawaida ya Soya na Samaki ambayo yanazidi kuwa ghali.
Shirika la chakula na kilimo duniani linabashiri kuwa kuongezeka kwa idadi ya watu duniani kutaongeza na mahitaji ya proteni inayotokana na Nyama na Samaki.
Hivyo basi kutakuwa na ushindani kati ya wanyama na binadamu, hususan katika mahitaji ya Proteni.
Kwa upande wa wanyama ongezeko la mahitaji ya proteni litafika asilimia 70 ifikapo mwaka 2050.
Hili litapunguza ardhi inayoweza fanyiwa ukulima na pia hifadhi za Samaki. Vyakula vya Samaki na Ng'ombe vyazidi kuwa ghali. Nafaka hutumika kutupa protini, lakini protini katika mimea haitoshi.
Funza
Soya ina protini za kutosha ila tu bei yake imekua ghali.
'Twahitaji vyakula mbadala.'
Aina tofauti ya Nzi, waweza kutumika kutengeza aina tofauti ya vyakula kwa kila hatua ya kukua katika maisha ya mnyama yeyote yule.
AgriProtein ilitangaza kuwa ilikua imekwisha changisha dola milioni 11, kwa matumizi ya ujenzi wa mashamba mawili ya kwanza ya kufuga nzi wa kuuzwa. Shamba la kwanza huko Cape Town litakua na Uwezo wa kutoa tani 20 ya buu na tani 20 za mbolea kila siku.
Wao hutumia aina tatu za Nzi akiwemo Yule wa kawaida wa nyumba, kila aina akiwa na aina tofauti ya vyakula anavyovila. Nzi wa kike na wale wa kiume hufugwa katika vizimba vikubwa na mayai yao kuchukuliwa kisha kuchanganywa na vyakula vyao.
Kilo moja ya mayai yao hugeuka kuwa takriban kilo 380 ya buu, katika muda wa siku tatu tuu. Buu hawa hutolewaa kisha kukaushwa na kusiagwa na kinachobakia hua ni mbolea iliyo na Naitrojini.
'Bidhaa za nzi'
Enterra Feed Corporation, kampuni ya huko Vancouver, ina mipangilio ya kuzalisha bidhaa za nzi weusi, mara tatu zaidi. Bidhaa hizi zitatumika kulisha wanyama wanaofugwa na kisha kuwa vyakula vya wanyama wa majini baadaye.

Nzi wanaopatikana katika matunda
EnviroFlight, ya huko Ohio, Marekani, pia yatoa vyakula vya samaki waliofugwa.Karibu na Paris, Ufaransa, Ynsect, yatarajiwa kufuga Nzi hao pia kwa kiwango kikubwa itimiapo mwaka 2016.
Protix Biosystems ya Uholanzi pia ina mipangilio ya kupanua ufugaji wao wa nzi na kuuza buu kwa maumizi ya vyakula vya wanyama nap protini.
Sheria katika sehemu zingine hata hivyo zinazuia ufugaji wa Nzi kwa ajili ya kutengeneza vyakula. Katika Muungano wa nchi za Uropa, Nzi huchukuliwa kama mifugo wanapouawa na kukaushwa au kutengenezwa kwa njia nyingune yoyote ile.
Hili lamaanisha kuwa protini yao yaweza kulishwa tu kwa wanyama ambao si wa kuliwa na binadamu. Wanyama wanaofugwa pia hawawezi lishwa kwa minajili ya kutoa mbolea tu.
Sheria hizi zilizotengenezwa katika miaka ya 1990, hazikutarajiwa kuhusisha nzi.
Je, watumizi watakubali vyakula kutoka kwa wanyama waliolishwa buu na funza? Binadamu hula kuku na samaki.
Kuku hula wadudu hawa na pia samaki wanaovuliwa majini hula wadudu hawa. Miaka 10 au 15 kutoka sasa, hili litakua tasnia kubwa ulimwenguni.

CHANZO: http://www.bbc.co.uk/swahili

Papa awapokea Peres na Abbas

 

 Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Francis amewakaribisha Rais wa Israil, Shimon Peres, na mwenzake kutoka Palestina, Mahmoud Abbas, katika maombi ya aina ya kipekee katika makao makuu ya Kanisa Katoliki ya Vatican. Viongozi hao wawili walikutana na Papa nje ya makaazi yake kabla ya kuandamana naye, wakiandamana na kiongozi wa Kanisa la Ordhodoz, Partriarch Artholomew kwa hafula maalumu katika Medani ya Vatican. Akiongea katika hafula hiyo Papa alisema ujasiri na nguvu vinahitjika katika juhudi za kuleta amani.
"Kuleta amani kunahitji ujasiri mkubwa kuliko vita. Kunahitaji ujasiri wa kusema ndio kwa mkutano na La kwa vita; ndio kwa mashauriano na La kwa makabiliano; ndio kwa kuheshimu mikataba na La kwa uchokozi; Ndio kwa ukweli na La kwa Uongo; kwa haya yote tunahitaji ujasiri na nguvu moyoni," Papa alisema

Na katika hotuba yake Bwana Peres alisema alitakia vizazi vyote vijavyo amani ya kudumu:
"Rafiki wapenzi, Nilikuwa mchanga, na sasa nimezeeka. Nilishuhudia vita, Nilionja amani. Sitawahi kusahau familia zilizofiwa, wazazi na watoto waliolipia gharama kubwa kwa vita hivyo. Na maisha yangu yote sitakoma kuitisha amani, kwa niaba ya vizazi vijavyo. Naomba sisi sote tuuungani mikono na kufurahi kwa sababu ni wajibu wetu kufanya hivyo kwa niaba ya watoto wetu.
Na kwa upande wake Bwana Abbas aliombea amani katika mkutano huo," alisema Peres.


Naye kiongozi wa Palestina, Mahmoud Abbas, aliomba kwenye hafula hiyo.


"Ee Bwana, tuletee amani ya kudumu na ya haki katika taifa letu na eneo letu, kwa ujumla, ili watu wetu na watu wote wa Mashariki ya Kati na Dunia nzima ifurahie matunda ya amani, utangamano na kuishi kwa pamoja kwa upendo.

Baada ya sherehe hiyo, iliyoshirikisha maombi ya Kikristo, Kiyahudi na Kiislamu, waliokuwepo walisalimiana kwa mikono na kupanda Mzaituni katika Medani ya Vatican kama ishara ya amani.

Papa ametangaza hadharani kuwa hataki kuingilia moja kwa moja mashauriano ya amani ya Mashariki ya kati, yaliyoporomoka Aprili lakini akasema kuwa anatarajia kwamba mkutano katika Vatican utapunguza uahasama kati ya pande hizo mbili kinzani za Mashariki ya Kati.

CHANZO: http://www.bbc.co.uk/swahili