Monday, September 2, 2013

KUMBUKUMBU YA MAREHEMU DAUDI MWANGOSI , MAANDAMANO YA WANAHABARI YATIKISA MJI WA IRINGA


Wanahabari  wa  vyombo  mbali mbali na  wadau  wa habari  mkoa  wa  Iringa  wakiwa katika  maandamano ya amani ya  kumuenzi  aliyekuwa mwenyekiti  wa klabu ya  waandishi  wa  habari  mkoa  wa Iringa (IPC) leo 
Maandamano  ya  wanahabari na  wadau  wa  habari yakipita  eneo la soko kuu la manispaa ya  Iringa 
Katibu  wa IPC  Francis  Godwin  akiongoza  maandamano ya  wanahabari na  wadau huku akiwa  juu ya gari na picha ya marehemu Daudi Mwangosi
Wanahabari  Iringa katika maandamano ya  kumuenzi  marehemu  Mwangosi  leo
 Maandamano ya  wanahabari  na  wadau  wa habari  mkoa wa Iringa ya  kumuenzi marehemu Daudi Mwangosi  yakipita  eneo ya  uhindini  


 Wananchi  wakishuhudia maandamano  hayo  leo





Katibu  mtendaji  wa IPC  Francis  Godwin akitoa taarifa ya  kuanza kwa maandamano ya kumuenzi marehemu Daudi Mwangosi leo
Katibu  wa  IPC Francis  Godwin mwenye pama akikabidhi maandamano ya  mwenyekiti  wa IPC Frank Leonard na  wadau  wengine  eneo la Maktaba ya  mkoa wa Iringa


Katibu  wa  IPC  FrancisGodwin kushoto akikabidhi picha ya marehdemu Daudi Mwangosi kwa  mwenyekiti  wa IPC  Frank Leonard kulia,wanaoshuhudia ni mzee  Fulgence  Malangalila  na Majid Mjengwa 


Mwenyekiti wa  IPC Frank Leonard  kushoto akikabidhi  picha ya  Mwangosi kwa mwasisi  wa IPC mzee Fulgence Malangalila 









MAANDAMANO ya  wanahabari  mkoa  wa  Iringa  kwa  ajili ya  kumbukumbu  ya  mwaka  mmoja wa  kifo  cha  aliyekuwa  mwenyekiti  wa klabu ya  waandishi  wa habari  mkoa  wa  Iringa (IPC) na mwandishi  wa Chanel  Ten Marehemu  Daudi Mwangosi  yatikisa mji  wa  Iringa leo.

Maandamano  hayo ambayo  yameanza majira ya saa 4 asubuhi  katika  viwanja   vya  bustani ya  Manispaa ya  Iringa yamepata  kuzungukakatika maeneo  mbali mbali ya  mji wa  Iringa kabla ya  kupokelewa na mwenyekiti  wa IPC  Frank Leonard katika  ukumbi wa maktaba ya  mkoa kwa mkutano wa  wadau  wa habari.

katika  maeneo  mbali mbali  ambayo maandamano  hayo yamepita  likiwemo  eneo la Uhindini , Mashine  tatu, Soko  kuu na stendi  kuu ya mabasi ya mikoani  wananchi  walilazimika  kusitisha  shughuli  zao kushuhudia maandamano  hayo ambayo yaliongozwa na  askari  wa  usalama barabarani .

CHANZO: www.francisgodwin.blogspot.com

No comments:

Post a Comment