![]() |
| .....Pichani Emmanuel akipatiwa matibabu kutokana na majeraha ya moto aliyopata. |
Mwanafunzi wa shule ya ufundi ya Nsambya nchini Uganda amejichoma moto baada ya kupoteza ada ya shule aliyopewa na baba yake.
Mwanafunzi huyo Emmanuel Ogabe, mtoto wa
Bw. Moses Ogabe hivi sasa anatibiwa majeraha hayo ya moto katika
hospitali ya Mulago ambako alikimbizwa baada ya kufanya jaribio hilo la
kujitoa uhai wake siku ya Jumanne usiku ambapo baba yake Mzee Ogabe
amesema mtoto huyo mara kadhaa amekuwa akijaribu kujiua.
Ogabe amesema alijaribu kujitoa uhai
wake kwasababu amekuwa akidai kutengwa na wazazi wake wakati
wanajitahidi kumpatia mahitaji yake hivyo hakuweza kuvumilia jinsi
atakavyomwangalia baba yake baada ya kupoteza shilingi laki moja za
Uganda alizopatiwa na baba yake.
Amesema alipogundua kuwa amepoteza pesa
hizo, kijana huyo alirejea nyumbani na kujitumbukiza ndani ya mafuta ya
taa kisha kujiwasha kwa kiberiti ambapo aliokolewa na baba yake ambaye
alimkimbiza na kuuzima moto huo kwa maji.

No comments:
Post a Comment