Monday, November 12, 2012

HII NDIO GENERATOR INAYOTUMIA HAJA NDOGO (MKOJO)


moja kati ya product ambayo haikutegemewa kabisa ni hii ya Genereta inayotumia haja ndogo (Mkojo) katika Maker Faire Africa mwaka huu huko Lagos Nigeria iliyotengenezwa na watoto wakike wanne ambao ni Duro-Aina Adebola (14), Akindele Abiola (14), Faleke Oluwatoyin (14) na Bello Eniola (15).



Lita moja ya mkojo inakupa masaa 6 ya umeme



Mfumo mzima unafanya kazi hivi:


  • mkojo unawekwa kwenye electrolytic cell ambayo inatenganisha Hydrogen
  • Hydrogen inakwenda kwenye filter ya maji kwa ajili ya kusafishwa ambapo baada ya hapo inasukumwa kwenda kwenye gas cylinder.
  • Gas cylinder inaisukuma Hydrogen kwenye cylinder ya liquid borax ambayo inatumika kuondoa moisture kwenye gas ya hydrogen
  • hii gas ya Hydrogen iliyosafishika inasukumwa na kuelekea kwenye generetor

No comments:

Post a Comment